Friday, October 8, 2010

Kigoma na Tabora

Mama Kikwete akipatiwa watoto mapacha yatima wa kiume na mama mlezi wa kituo cha kulelea yatima kilichopo kijiji cha Matyazo Kigoma.

Mama Salma Kikwete Oyeeee! wanawake wa kijiji cha Nguruka Kigoma Kusini wakimshangilia Mama Kikwete
 Jamani eee Kigoma neema ! hii ndio faida ya kilimo !wakulima wa kijiji cha Mtalima Kasulu.


 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akimnadi Mgombea Ubunge Samuel Sitta.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akimnadi mgombea (CCM)jimbo la Kigoma Mjini Peter Serukamba.

 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akisalimia katika kijiji cha Mvugwe kiliopo halmashauri ya Kasulu (Kigoma) wakati akielekea Kigoma.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akizungumza katika mkutano wa ndani wa kampeni jimbo la Kasulu vijijini

Mama Kikwete akiwahutubia wanawake wa Kaliua (jimbo la Urambo Magharibi)Tabora katika mkutano wa ndani wa kampeni
 Mama Salma Kikwete akimnadi mgombea ubunge jimbo la Urambo Magharibi Prof. Juma Kapuya
 Mama Salma Kikwete akiwahutubia akina mama wa UWT Urambo Mashariki (Tabora)
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akipokea shada la maua alipowasili Jimbo la Urambo Mkoani Tabora

Saturday, October 2, 2010

CCM inafanana na Mti wenye Matunda

Na Mwaandishi Maalum,Mtwara:
Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA), Mama Salma Kikwete, amekifananisha Chama Cha Mapinduzi na mwembe ambao hurushiwa mawe kutokana na matunda yake. Alisema wapinzani wanaisema CCM kwa sababu serikali imefanya mambo mazuri kwa ajili ya maendeleo ya wananchi na taifa baada ya kutekeleza kwa mafanikio ilani ya uchaguzi ya chama hicho ya 2005. “Ukiona wapinzani wanaisema sana CCM ujue imefanya mambo mazuri, ni sawa na mwembe wenye matunda hupigwa mawe, kwani umeshaona mwembe usio na matunda ukipigwa mawe,” alihoji. Mama Salma alisema hayo jana na juzi alipokuwa akizungumza kwa wakati tofauti na wanachama wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) katika mkoa wa Mtwara. Kuhusu uchumi, aliwaambia uuzaji wa mazao kwa mfumo wa stakabadhi ghalani ni ukombozi kwa wakulima dhidi ya walanguzi. Taarifa iliyowasilishwa kwake ilieleza kwamba, uuzaji korosho kwa mfumo huo umewanufaisha wakulima ambao hulipwa malipo kwa awamu mbili hadi tatu kulingana na bei ya soko. Ilieleza kwamba, wakati serikali ya awamu ya nne inaiingia madarakani kilo moja ya korosho ilikuwa ikiuzwa kwa kati ya sh. 150 hadi 300, kwa sasa ni sh. 800 hadi sh.1000 kwa mfumo wa stakabadhi ya mazao ghalani. Mama Salma alisema wanaoupinga mfumo huo, wanataka kuendelea kujitajirisha kwa jasho la wakulima kama ilivyokuwa huko nyuma. “Msidanayike, uuzaji wa mazao kwa stakakabadhi ya mazao ghalani ni ukombozi kwa wakulima, na serikali ya CCM inawapenda haiwezi kuwadhulumu ndiyo maana inasisitiza na kusimamia mazao kuuzwa kwa vyama vya ushirika,” alisema na kupigiwa kofi na vigelegele. Wakati akiwanadi wagombea ubunge Mariam Kasembe (Masasi), Jerome Bwanausi (Lulindi), George Mkuchika (Newala), Juma Njwayo (Tandahimba), Hawa Ghasia (Mtwara Vijijini) na Mohamed Murji (Mtwara Mjini), Mama Salma alitoa wito kwa wanawake viongozi kupigania kwa dhati maendeleo ya kina mama wenzao. Alisema haipendezi mwanamke kiongozi kuwa kikwazo katika maendeleo ya wenzake, alibainisha Mama Salma na kushangiliwa na kina mama hao.

Sunday, September 26, 2010

Serikali imetekeleza ilani ya uchaguzi ya 2005 kwa mafanikio makubwa.

Na Mwandishi Maalumu, Lindi
MWENYEKITI wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA), Mama Salma Kikwete, amewataka wanachama wa CCM kutembea kifua mbele kwa sababu serikali imetekeleza ilani ya uchaguzi ya 2005 kwa mafanikio makubwa.Alisema hayo alipozungumza kwa nyakati tofauti jana na juzi na wanachama wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) katika majimbo ya Kilwa Kaskazini, Kilwa Kusini, Mchinga, Mtama, Lindi Mjini, Ruangwa na Nachingwea.Mwenyekiti huyo alisema kama yalivyo maeneo mengine nchini, ndivyo ilivyo katika majimbo hayo kwa maendeleo yaliyopatikana katika miaka mitano ya serikali ya awamu ya nne hali inayodhihirisha utekelezaji mzuri wa ilani hiyo.“Hivi mtu anapotoka huko na kusema CCM haijafanya lolote, alitaka ifanye nini? Wana-CCM tembeeni kwa kujidai kwa sababu katika kipindi cha miaka mitano serikali imefanya mambo mengi mazuri kwa maendeleo ya nchi yetu,” alisema na kupigiwa kofi.Taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya CCM ya 2005 katika majimbo hayo ilitaja baadhi ya maendeleo yaliyopatikana ni kuongezeka kwa wanafunzi wanaoingia kidato cha kwanza, kuboreka kwa barabara, huduma ya maji na kina mama kuwa na mwamko wa kujishughulisha na miradi inayowaingizia pesa.Mfano, katika wilaya ya Kilwa wanafunzi wanaojiunga na kidato cha kwanza wamefikia 6,300 ikilinganishwa na 1,280 wa mwaka 2005, shule za sekondari zilikuwa nne kwa sasa ziko 25 huku idadi ya walimu ikiongezeka kutoka 35 na kufikia 128.Wilaya ya Kilwa kwa miaka mingi ilikuwa na tatizo sugu la upatikanaji wa umeme lakini kwa sasa shida hiyo ni historia baada ya kuwa na umeme wa uhakika unaotokana na gesi ya Songosongo.Mama Salma alisema, kwa mafanikio hayo ni wazi CCM itashinda kwa kishindo katika uchaguzi, na kuwataka kina mama kutopoteza kura zao kwa kukivipigia kura vyama vya upinzani ambavyo haviwezi kushinda katika uchaguzi uliopangwa kufanyika Oktoba 31, mwaka huu.Aliwataka wazazi kuwasimamia watoto wao wasome kwa bidiii kwa sababu elimu ndiyo msingi mkuu wa maendeleo kwa nchi yoyote.“Mtu asikudanganye, nchi zote zilizopiga hatua katika maendeleo zimewekeza katika elimu kwa vijana wao, na ndicho serikali imekifanya katika miaka mitano hii,” alisema.Alisema baada ya ujenzi wa shule za sekondari za kata kutia for a, ni dhamira ya Chama Cha Mapinduzi kuona wanaomaliza kidato cha nne wanaendelea kupata elimu ya kidato cha tano na sita, hivyo kila tarafa itajengwa shule yenye vidato hivyo.Alikemea tabia ya undumila inayoonyeshwa na baadhi ya viongozi na wanachama wa CCM, akisema isipoachwa itakikosesha ushindi wa kishindo katika uchaguzi.“Wengine hapa mchana wamevaa kijani, usiku wako kwenye vyama vingine, kweli au si kweli,” alihoji Mama Salma na kujibiwa kwa sauti “kweli, sema mama.” Aliwasihi viongozi na wanachama waondoe tofauti miongoni mwao na kuwa kitu kimoja kuwezesha ushindi mkubwa kwa CCM, kwani kuendelea na hali ya kutofautiana ni kutoa upenyo kwa wapinzani.





Friday, September 17, 2010

Ushirikiano ni nguzo muhimu

Misungwi

MWENYEKITI wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA), Mama Salma Kikwete, amewaambia viongozi wa Chama Cha Mapinduzi kuwa, ushindi wa kishindo katika uchaguzi mkuu utapatikana iwapo watafanyakazi kwa ushirikiano.Alisema hayo juzi na jana alipozungumza kwa nyakati tofauti na wanachama wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), katika wilaya za Geita, Sengerema, Kwimba na Misungwi, mkoani Mwanza.Mama Salma alisema kuna taarifa kwamba, baadhi ya maeneo viongozi wa CCM wapo katika ofisi moja lakini hawazungumzi wamenuniana kutokana na sababu mbalimbali.Alisema miongoni mwa sababu hizo ni matokeo ya kura za maoni za kuwapata wagombea wa udiwani na ubunge zilizopigwa Agosti 1, mwaka huu, ambapo baadhi ya viongozi waliwaunga mkono wagombea ambao walishindwa,hivyo kubaki na kinyongo."Kuna mahali katibu na mwenyekiti hawazungumzi, wamenuniana, kweli hapo kazi itafanyika?" Alihoji Mama Salma na kina mama kumuitikia kwa kusema "haifanyiki."Katika kuonyesha kuguswa na hilo, kina mama hao walikuwa wakikatisha hotuba ya Mama Salma kwa kusema "sema mama, waambie hao."Mama Salma alisema kwamba, ana uhakika CCM itashinda katika uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba 31,mwaka huu, lakini ushindi huo lazima uwe wa kishindo, na utapatikana kwa viongozi wa CCM na wanachama kuwa kitu kimoja katika mchakato wa kampeni hadi siku ya kupiga kura.Taarifa zilizowasilishwa kwake na makatibu wa UWT katika wilaya hizo, zilisema moja ya matatizo yaliyopo ni makundi miongoni mwa viongozi na wanachama yaliyosababishwa na matokeo ya kura za maoni.Mama Salma alissisitiza kwamba,  katika mchakato huo wa kura za maoni ilikuwa ni lazima wagombea kuwa na wanaowaunga mkono, kwani ingekuwa ni kituko kwa mtu kutangaza nia na kugombea asiwe na watu wanaomuunga mkono katika azma yake hiyo."Hivi wewe unaposema huyu hakuwa wangu, wakati chama kimeshateua mgombea, unamaanisha nini? Unafanya hivyo kwa masilahi ya nani? Tusifanye makosa, kwenye mambo ya msingi hatufanyi majaribio," alionya Mama Salma.Aliwaambia kina mama hao kwamba, wana kila sababu ya kujisikia fahari na Chama Cha Mapinduzi kwa namna serikali ilivyotekeleza yale yaliyoahidiwa kwenye ilani ya uchaguzi.Miongoni mwa yaliyoahidiwa na kutekelezwa, ni ujenzi wa shule za sekondari, ujenzi wa barabara, na kwa wilaya hizo ni ununuzi na ukarabati wa vivuko vinavyofanya kazi ya usafirishaji wa abiria na bidhaa katika Ziwa Victoria.Mama Salma aliwanadi kwa kina mama hao, wagombea ubunge wa CCM, Dk. Charles Tizeba (Buchosa), Donald Max (Geita), Lorensia Bukwimba (Busanda), Richard Ndassa (Sumve) na Sharif Mansoor (Kwimba). Mbunge wa Sengerema ambaye pia ni Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja hana mpinzani.Mama Salma yuko katika ziara ya kuwatembelea wanachama wa UWT kuwahamasisha kujitokeza kwa wingi katika uchaguzi mkuu na kuwapigia kura wagombea wa CCM kwa mtindo maarufu wa 'mafiga matatu.'

Wito kwa wagombea waliokosa wapinzani

NA MWANDISHI MAALUMU, KONGWA
 MWENYEKITI  wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA), Mama Salma Kikwete, amewataka wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambao katika kata na majimbo yao wagombea wamepita bila kupingwa, wasibweteke, waendelee kufanya kampeni za nguvu kukiwezesha chama kupata  ushindi wa kishindo katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 31, mwaka huu.Mama Salma alisema hayo Agosti 29, 2010,  alipozungumza na wanawake wa wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma, akiwa katika ziara ya siku mbili mkoani humo kuwahamasisha wanawake kujitokeza kwa wingi kupiga kura katika uchaguzi huo.Mwenyekiti huyo wa WAMA aliwaomba kinamama hao kuwachagua wagombea wa CCM kwa mtindo maarufu wa chama hicho wa mafiga matatu, yaani diwani, mbunge na rais.Taarifa ya chama hicho wilayani Kongwa, ilieleza kwamba mbunge anayetetea nafasi yake katika jimbo la Kongwa, Job Ndugai wa CCM, amekosa mpinzani, na wagombea udiwani nane kati ya 22 nao wamepita bila kupingwa.Taarifa hiyo ilieleza kuwa, Ilani ya Uchaguzi ya CCM imetekelezwa Kongwa kwa zaidi ya asilimia 85, ambapo kwa upande wa shule za sekondari zimeoongezeka kutoka tano mwaka 2005 hadi kufikia 24, huku baadhi ya kata zikiwa na shule tatu za sekondari kulingana na idadi ya wanafunzi wa maeneo husika.Kutokana na ongezeko la shule hiyo, taarifa hiyo iliyowasilishwa na Mwenyekiti wa CCM wa wilaya ya Kongwa, Abdi Matali, ilisema wanafunzi wanaojiunga na elimu ya sekondari nao wameongezeka kutoka 1,324 mwaka 2005 hadi kufikia 9,850.Mama Salma alisema kwamba, CCM ina kila sababu ya kuchaguliwa kuendelea kushika dola kwa sababu imetekeleza kwa mafanikio makubwa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2005 iliyonadiwa nchini kote na kukubaliwa na wananchi.

Monday, September 13, 2010

Mama Salma apongezwa kusaidia wanawake

 NA MWANDISHI MAALUMU, MUSOMA
WANACHAMA wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), mkoa wa Mara, wamempongeza Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA), Mama Salma Kikwete, kwa jitihada zake za kushughulikia kero zinazowakabili wanawake pasipo kujali itikadi.Katika taarifa za utendaji kazi zilizowasilishwa kwake Septemba 13,2010, na makatibu wa UWT wa wilaya za Musoma Mjini, Musoma Vijijini na Bunda, mkoani humo, zilieleza kwamba Mama Salma amewasaidia wanawake kujikwamua kiuchumi pamoja na kupigania elimu kwa watoto wa kike. Makatibu hao, Agness Methew (Bunda), Ashura Kimwaga (Musoma Mjini) na Hamisa Chacha (Musoma Vijijini), kwa nyakati tofauti walisema kwamba bila kujali itikadi amekuwa akiwawezesha kiuchumi kina mama katika vikundi vyao vya uzalishaji mali.
 Watendaji hao wa UWT walimsifu Mama Salma kwa kuwa mstari wa mbele kupigania elimu kwa watoto wa kike, jambo ambalo ni ukombozi katika maisha yao ya baadaye.Mama Salma ambaye yuko mkoani Mara kuwahamasisha wanawake kujitokeza kwa wingi kwenye uchaguzi mkuu Oktoba 31, mwaka huu, na kuwapigia kura wagombea wa Chama Cha Mapinduzi, alisema kwamba, Ilani ya CCM ya 2005 ilizungumza kuwawezesha kina mama kiuchumi, na kuwapatia nafasi katika vyombo vya maamuzi, mambo ambayo yametekelezwa kwa kiwango kikubwa.Alifafanua kwamba uwezeshaji kiuchumi kwa wanawake umefanyika kupitia vyama vya ushirika (SACCOS) hatua ambayo imewapa uwezo wa kumudu gharama za mahitaji yao na ya familia zao.Mama Salma aliwakumbusha kina mama hao kwamba, kwa kuwa fedha zinazotolewa kupitia SACCOS ni mikopo, ni muhimu kwa kila anayezikopa kuzirejesha kwa wakati kuwezesha wengine kutumia fursa hiyo na kujikwamua kiuchumi. “Licha ya wanawake kuwezeshwa kiuchumi katika kipindi hiki cha miaka mitano, pia wengi wapo katika ngazi za maamuzi,” alisema.Mama Salma aliwataka wanachama wa CCM kuyatangaza mafanikio ya utekelezaji wa Ilani ya CCM ya 2005 pasipo woga, kwa sababu mengi yaliyoahidiwa yametekelezwa kwa asilimia kubwa.Alifafanua kwamba, katika harakati za kuleta maendeleo, changamoto haziwezi kukosekana na kutoa mfano kwamba, mafanikio katika ujenzi wa shule za sekondari katika kila kata nchini, yameibua upungufu wa walimu, maabara na nyumba za kuishi watumishi hao.Mama Salma alisema serikali inazifahamu changamoto hizo, na ndiyo msingi wa kuongeza bajeti ya elimu kuwezesha kutatuliwa na kuwepo kwa wanafunzi wengi wanaosomea ualimu katika vyuo mbalimbali kikiwemo Chuo Kikuu cha Dodoma ambapo katika chuo chake cha ualimu, kila mwaka kitakuwa kikitoa wahitimu wa ualimu 15,000 hatua ambayo itaoondoa tatizo la watumishi hao nchini kote katika kipindi kifupi kijacho.Aliwasihi Watanzania wasidanganyike na kauli za wapinzani kwamba watakapoingia madarakani kila kitu kitakuwa bure, na hawatatoza kodi.“Hakuna serikali yoyote hapa duniani inayoendeshwa pasipo kutoza kodi. Tusidanganyike,” alisema na kuitikiwa; “hatutadanganyiki.” Mama Salma aliwanadi wagombea ubunge kupitia CCM, Stephen Wassira (Bunda) na Vedastus Mathayo (Musoma Mjini). Mbunge wa Musoma Vijijini Nimrod Mkono amepita bila kupingwa.Tayari Mama Salma ameshafanya ziara kama hiyo na kuzungumza na kina mama kwenye mikutano ya ndani, katika mikoa ya Pwani, Dodoma, Singida, Manyara na Dar es Salaam.

Uhamasishaji wa ushiriki katika uchaguzi mkuu mkoani Mara

Mwenyekiti wa Taasisi ya Maendeleo ya Wanawake (WAMA) Mama Salma Kikwete akisalimiana na Wanachama wa UWT Mkoa wa Mara Sept.12,2010 alipowasili kwenye uwanja wa ndege wa Musoma . Mama Salma Kikwete yupo mkoani hapo kwa ajili ya kukutana na wanachama wa UWT katika mikutano ya ndani kuhusu kuwahamasisha umuhimu wa kupiga kura katika Uchaguzi Mkuu Ujao mwaka huu.(kulia) Mwenyekiti wa UWT mkoa Mara Nancy Sessani. (Picha na Mwanakombo Jumaa)














Chini;Katibu wa UWT Mara Helena Chacha akimkaribisha Mwenyekiti wa WAMA baada ya kuwasili Mkoani hapo kwa ziara ya kuwahamasisha ushiriki katika uchaguzi.














Mama Salma akifurahia ngoma ya asili wakati alipowasili Musoma 12,9,2010.

Tuchambue Kauli Za Wanasiasa

 WATANZANIA wameaswa kuyachambua kwa umakini yanayozungumzwa katika kampeni za kisiasa wakati huu wa kuelekea uchaguzi mkuu ili kung’amua ukweli na uongo.Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA), Mama Salma Kikwete, alisema hayo wiki hii mjini Dar es Salaam, alipokuwa akizungumza na wanachama wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT).Alisema katika kipindi hiki cha kampeni yatazungumzwa mengi, ikiwa ni pamoja na ahadi zisizotekelezeka kama za utoaji wa elimu bure kuanzia chekechea hadi chuo kikuu na kufuta kodi.“Tuwasikilize, tupembue chuya zikae upande wake, chenga upande wake na mchele ukae upande wake, tuseme lilo la kweli, kama serikali haitatoza kodi, itaendeshaje shughuli zake?” Alihoji na kujibiwa “hatudanganyiki mama”. Mama Salma ambaye kitaaluma ni mwalimu, alisema gharama zinazotozwa na serikali kwa wazazi na walezi katika elimu, ni ndogo sana ikilinganishwa na za nchi nyingine.Akizungumzia baadhi ya mafanikio yaliyopatikana katika sekta ya elimu, Mama Salma kwa kiwango kikubwa yameboreshwa ikilinganishwa na wakati wake alipokuwa akifundisha.Alisema kwa miaka zaidi ya miaka 15 ambayo amefanya kazi ya ualimu, maslahi ya walimu yalikuwa duni, lakini katika kipindi cha miaka mitano ya serikali ya awamu ya nne yameboreshwa ikiwa ni pamoja na walimu kupandishwa na madaraja na mishahara kuongezeka.‘’Nimefundisha kwa miaka 16 mshahara wangu ulikuwa hauzidi sh. 150,000, lakini kwa sasa hali siyo hiyo, yamefanyika maboresho makubwa katika masilahi ya walimu,” alisema.Mama Salma alisema kuongezeka kwa shule za sekondari nchini, ni uthibitisho kwamba serikali ina dhamira ya dhati ya kuwaletea wanachi maendeleo kwa sababu nchi zilizoendelea zimewekeza katika elimu ya watoto na vijana wao.Aliwasisitizia wanachama wa Chama Cha Mapinduzi kutokuona aibu ya kuelezea mafanikio yaliyopatikana katika utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya 2005.

Sunday, September 12, 2010

WAMA's take on Orphans and Vulnerable Children (OVC)


 
The growing number and need for orphans and vulnerable children in Tanzania due to HIV/AIDS is becoming a major concern. The program vision is to see improved and strengthened best initiatives based on community mode for caring and support for OVC by making all stakeholders including community in itself, are playing their role equally and in an effective way.
This Program has developed and maintains a working relationship with the Ministry of Health and Social Welfare, and the Ministry of Community Development, Gender and Children, Ministry of Labour, Employment and Youth Employment, Ministry of Local Government, USAID and PACTCurrently WAMA is working on creating a database of OVCs and community based programmes for supporting OVCs. The Program is also liaising with key stakeholders to develop a strategy that will enable the Foundation to make interventions under the revised National Child development Policy of 2000.
The program uses various strategies such as strengthen and support the capacity of families to protect and care for OVC. Mobilize and strengthen community based responses to care, support and protection of orphans and vulnerable children and raise awareness and advocate for the creation of a supportive environment for orphans and vulnerable Children .
The program carries out the following activities :
• Provide psychosocial support within families to improve the wellbeing of OVC by providing training programme that address holistic needs of OVCs.
• Provide material support to OVCs
• Establish food security schemes for OVC and their families to improve nutrition and health of OVCs and their families through community food banks.
• Support Vocational and skills training to improve coping mechanism and functioning skill of child headed households by providing skills training programmes for child headed households on money management, food management nutrition and health, skills on parenting, decision making, and self awareness.
• To establish and maintain data base of OVC to identify needs priorities by developing OVC register, and establish directory of support priorities.
• To mobilize and organize for early identification of OVC
• Advocating for the rights of child at every level of society.
The Program has made the following achievements:
• Sponsored 21 orphans both boys and girls at Secondary, Primary and Vocational education.
• Enhanced learning among disabled children who are studying at Salvation Army, Tumaini Primary School by WAMA providing a Television set .
The units' Motto : We Stand for Children. Make a new dream for them


Zingatieni masharti mikopo isaidie wengi

NA MWANDISHI MAALUM, RUFIJI
WANAWAKE wanaokopa kutoka taasisi za fedha, wamekumbushwa kuzingatia masharti ya mikopo ikiwa ni pamoja na kuirejesha kwa wakati kuwezesha wengine kutumia fursa hiyo.
Akizungumza na kina mama wa wilaya za Mkuranga, Bagamoyo na Rufiji, mkoani Pwani, Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA), Mama Salma Kikwete, alisema kukopa fedha na kutozirejesha ni kukwamisha jitihada za wengine ambao nao wanazitaka kwa ajili ya kujikwamua kiuchumi.
Mama Salma alisema kwamba, mtu anapokopa fedha kwa ajili ya kutekeleza mradi, ahakikishe anazitumia kwa kazi hiyo na sio vinginevyo."Kina mama wenzangu, mkopo ni mkopo, lengo lilokufanya uchukue mkopo ni mradi wa kujiletea maendeleo, usitumie fedha za mkopo kununua doti za khanga, huko ni kujisababishia matatizo bila sababu za msingi," alisema.Alifafanua kwamba, serikali ya awamu ya nne ilipoingia madarakani ilikuwa na kauli mbiu ya maisha bora kwa kila Mtanzania, na fursa ya kupata mikopo, inalenga katika kuwezesha kauli mbiu hiyo kutekelezeka.Mama Salma aliwasisitizia wanawake kuendelea kujiunga na vyama vya kuweka na kukopa (SACCOS) na VICOBA, ili kujiweka katika mazingira mazuri ya kupata fedha za mikopo kwa ajili ya kuendeleza na kuanzisha miradi ya uzalishaji mali.Kuhusu elimu, alisema mataifa yote yaliyoendelea, yamewekeza katika elimu ya watoto wao ndiyo maana serikali chini ya uongozi wa Rais Jakaya Kikwete katika miaka mitano yakuwepo madarakani, iliamua kujenga shule nyingi za sekondari na kupanua elimu ya vyuo na vyuo vikuu.Huku akiwaomba kina mama hao kumpigia kura mgombea urais wa CCM Rais Jakaya Kikwete na wagombea wa ubunge na udiwani wa chama hicho katika uchaguzi mkuu ulipangwa kufanyika Oktoba 31, mwaka huu, Mama Salma alisema miaka ya sasa siyo ya kupuuzia elimu."Nchi yoyote yenye mafanikio imewekeza vyema katika elimu ya watoto wao, nasi hatuwezi kubaki nyuma katika hilo, shule nyingi tumejenga kwa nguvu zetu na msaada wa serikali, lakini pia tunakabiliwa na changamoto nyingi kuziwezesha kuwa bora zaidi," alisema."Mkikichagua tena Chama Cha Mapinduzi kitafanya kazi hiyo kwa ari zaidi, nguvu zaidi na kasi zaidi," alisema.

Thursday, September 9, 2010

Anayependa maendeleo atatambua mafanikio ya serikali-Mama Salma

MWENYEKITI wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA), Mama Salma Kikwete, amesema mtu anayependa maendeleo nchini, atatambua mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha miaka mitano ya uongozi wa serikali ya awamu ya nne. Akizungumza kwa nyakati tofauti na wanawake wa wilaya za Kibaha, Chalinze na Bagamoyo, mkoani Pwani jana {24.8.2010}, alisema mengi yaliyoahidiwa na Chama Cha Mapinduzi katika uchaguzi mkuu wa 2005, yametekelezwa. Mama Salma Kikwete alisema, katika suala la maendeleo na mustakabali wa nchi, ni lazima wanawake waangalie ni chama gani chenye sera na ilani makini, katika kuwaletea maendeleo yao, na jamii yote ya Watanzania. Alitaja baadhi ya mafanikio yaliyopatikana katika kipindi hicho kuwa ni ujenzi wa shule za sekondari za kata, zilizoondoa tatizo la watoto wanaofaulu na kushindwa kuendelea sekondari kwa kukosa nafasi. Mama Salma alisema, ujenzi wa shule za sekondari umeongezeka kutoka 1,745 hadi 4,102 katika kipindi cha miaka mitano, jambo ambalo ni mafanikio makubwa, lakini kuna watu wanaojifanya kutoyaona. Kutokana na kuongezeka kwa shule hizo, alisema idadi ya wanafunzi nayo imeongezeka ambapo uandikishaji wa kidato cha kwanza hadi cha nne ulitoka kuwa wanafunzi 401,598, mwaka 2005, hadi 1,401,559 mwaka 2009. Kuhusu miundombinu, alisema ujenzi wa barabara zinazounganisha mikoa na wilaya nchini umewezesha wananchi kusafiri kwa haraka kutoka sehemu moja ya nchi kwenda nyingine, ikilinganishwa na hali ilivyokuwa huko nyuma. "Zamani ilikuwa kutoka hapa (Kibaha), hadi Lindi tulilazimika kulala njiani, lakini sasa mambo ni mazuri," alisema na kupigiwa kofi. Alisema, Chama Cha Mapinduzi kimetekeleza ilani yake kwa mafanikio makubwa, na asiye na macho haambiwi tazama, kwani wengine wanaona mafanikio hayo lakini wanajifanya hawaoni," alisema. Mama Salma aliwaomba kina mama hao kuwachagua wagombea wa Chama Cha Mapinduzi katika uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba 31, mwaka huu katika mtindo maarufu wa CCM wa mafiga matatu. "Siku ya tarehe 31 mwezi wa kumi, ukifika kituoni piga kura kwa mgombea urais wa CCM, mgombea ubunge wa CCM na mgombea udiwani wa CCM hayo ndiyo mafiga matatu," Alisema. Akizungumzia kura za maoni za CCM kuwapata wagombea ubunge na udiwani, Mwenyekiti wa WAMA alisema, zilisababisha makundi tofauti kwa sababu wagombea walikuwa ni wengi. Kwa vile mchakato huo umemalizika na wagombea kupatikana, aliwasihi wanachama wa CCM kuvunja makundi hayo na kuwa na kundi moja la CCM kwa ajili ya kukipatia Chama Cha Mapinduzi ushindi wa kishindo katika uchaguzi mkuu ujao. Kesho, (Agosti 25, 2010) Mama Salma Kikwete ataendelea na ziara ya kuzungumza na wanawake katika wilaya za Kisarawe, Mkuranga na Rufiji, na Agosti 26, 2010 anatarajiwa kuwa Mafia.